Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM leo limetoa wito wa kupewa fursa ya haraka ya kibinadamu kwenye kituo cha mahabusu cha wahamiaji kwenye mji mkuu wa Yemen, Sana'a ambako moto mkubwa umeripotiwa kusababisha vifo, majeruhi na uharibifu mkubwa mwishoni mwa wiki.