Kutokomeza nyuklia ni kuachana nazo kabisa- Guterres
Njia pekee ya kutokomeza tishio la silaha za nyuklia duniani ni kuachana kabisa na silaha hizo, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wakati akihutubia mkutano wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, kando mwa mjadala mkuu wa baraza hilo jijini New York, Marekani.