17 MEI 2023
Jaridani hii leo tunaangazia machafuko nchini Sudan na mchakato wa uchaguzi nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Kenya na Mashinani yunasalia hapa makao makuu kusikia ujumbe kuhusu idadi ya watu duniani.
Jaridani hii leo tunaangazia machafuko nchini Sudan na mchakato wa uchaguzi nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Kenya na Mashinani yunasalia hapa makao makuu kusikia ujumbe kuhusu idadi ya watu duniani.
Data mpya zinaonesha wasiwasi kuhusu ongezeko la idadi ya watu umeenea na serikali duniani zinazidi kupitisha sera zinazolenga kuinua, kupunguza au kudumisha viwango vya uzazi. Lakini juhudi za kushawishi viwango vya uzazi mara nyingi hazifanyi kazi na zinaweza kumomonyoa haki za wanawake, kwa mujibu wa ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu duniani UNFPA kuhusu Hali ya Idadi ya Watu Duniani.
Hii leo jaridani tunamulika masuala ya idadi ya watu na amani Sudan Kusini. Katika idadi ya watu ikiwa leo ni siku ya idadi ya watu duniani tunajulishwa kuwa ifikapo tarehe 15 mwezi Novemba mwaka huu idadi ya watu duniani itafikia bilioni 8! Na miongoni mwa nchi ambazo idadi ya watu inaongezeka ni Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Katika masuala ya amani huko Sudan Kusini mafunzo yameendeshwa ili jamii iweze kuwa sehemu ya kukabiliana na ukatili ikiwemo wa kingono. Makala inakupeleka Mexico kwa msichana ambaye ndoto yake ya kuwa mkunga ili kusaidia jamii yake imetimia.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya idadi ya watu duniani, shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu, UNFPA limeangazia jinsi ambavyo janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 limeingilia na kutishia fursa ya watu kuchagua kuwa na watoto au la.
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la idadi ya watu duniani UNFPA imesema ili kukabiliana na janga la kimyakimya la mila potofu hatua za haraka zinahitajika kukomesha ukeketaji (FGM), ndoa za utotoni na mila zingine ambazo zinathiri wanawake na wasichana.
Idadi ya watu duniani inatarajiwa kufikia bilioni 9.7 ifikapo mwaka 2050 na inaweza kuongezeka kwa kasi zaidi na kufika bilioni 11 mnamo mwaka 2100 kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa inayotathimini ongezeko la idadi ya watu duniani.
Mkutano wa 52 wa kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu idadi ya watu na maendeleo, CPDC umeng’oa nanga leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani.
Mkutano wa 52 wa kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu idadi ya watu na maendeleo, CPD umeng’oa nanga leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani.
Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya idadi ya watu imeonyesha bayana uhusiano mkubwa kati ya idadi ya watoto na na fursa ya mtu kupata haki ya msingi ya huduma za afya ya uzazi.