Katika maadhimisho ya siku ya saratani duniani hii leo, shirika la afya ulimwenguni WHO limeangazia kwa kina saratani ya shingo ya kizazi huku ikisisitiza umuhimu wa kuchunguzwa, kupokea chanjo ya Human Papiloma Virus, HPV na kutokomeza kabisa saratani ya shingo ya kizazi.