Skip to main content

Chuja:

Houthi

18 JUNI 2021

Katika jarida la mada kwa kina la Umoja wa Mataifa hii leo Assumpta Massoi anakuletea

-Mamilioni ya wakimbizi kuendelea kukabiliwa na njaa endapo msaada wa fedha za msaada hautopatikana limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP

-Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR imesema inatiwa wasiwasi miubwa na kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya raia na miundombinu yao kwenye jimbo la Marib nchini Yemen, mashambulizi yanayofanywa na kundi la Houthi

Sauti
13'3"
Mtoto huyu pichani mwenye umri wa miezi miwili ni mkazi wa Hajjah, nchini Yemen na ana unyafuzi. Mzozo unaoendelea nchini Yemen unasababisha mamilioni ya watu wawe hatarini kukumbwa na baa la njaa.
WFP/Marco Frattini

Chakula cha msaada Yemen chauzwa sokoni- WFP

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakuka WFP linataka kukomeshwa mara moja kwa hatua ya kupelekwa kwingine msaada wa chakula nchini Yemen baada ya kugundua mchezo mchafu unaofanywa katika mji mkuu wa Sana’a  na sehemu zingine zinazosimamiwa na kundi la Houthi wa kupeleka chakula maeneo yasiyokuwa yamelengwa na msaada huo.