Changamoto ya homa ya uti wa mgongo inaendelea Niger: WHO
Homa ya uti wa mgongo au meningitis imeendelea kuiathiri Niger kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO ambapo hadi kufikia tarehe 27 Januari 2023 kulikuwa na wagonjwa 559 huku 111 wakithibitishwa na vipimo vya maabara na idadi ya waliokufa kufa ni 18.