Ni jukumu la kila mtu kuzungumza na kuendeleza kumbukumbu ya Holocaust: Katibu Mkuu wa UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres Jumamosi ya leo akishiriki katika sinagogi ya Park East jijini New York Marekani katika maadhimisho ya kusherehekea ukombozi wa kambi ya mateso ya Auschwitz; amesema ni jukumu la kila mmoja kuenzi kumbukumbu za waliofariki katika mauaji ya maangamizi makubwa au Holocaust dhidi ya wayahudi.