Skip to main content

Chuja:

Hewa ya ukaa

28 Juni 2022

Karibu kusikiliza jarida ambapo wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari ukiendelea mjini Lisbon, Ureno kujadili suluhu za kukabiliana na changamoto za bahari tunakuleta mada kwa kina ikimulika eneo la Vanga Kilifi huko Kenya wanachi wamepata moja ya suluhu kubwa ambayo ni kuvuna na kuuza hewa ukaa kutoka kwenye mikoko kupitia mradi wa Vanga Blue Forest VBF, ambao kwa kiasi fulani unafadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP. 

Sauti
11'40"
Wingu katika eneo la Plechotice, Slovakia
WMO/Monika Nováková

Ripoti ya WMO yabaini ongezeko la hewa chafuzi katika anga

Ripoti ya shirika la hali ya hewa duniani WMO iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi imeonesha ongezeko zaidi la hewa chafuzi katika anga. Hali hii inayoendelea kwa muda mrefu  inaamaanisha kuwa vizazi vijavyo vitakabiliana na ongezeko la matokeo mabaya ya mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ongezeko la joto, mabadiliko makubwa ya hali uya hewa, upungufu wa maji, kuongezeka kwa kina cha bahari na uharibifu kwa viumbe wa majini na ardhini.

Tuwe makini maendeleo yasisababishe zahma- Lajčák

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Miroslav Lajčák aliyeko ziarani nchini Kenya, amesema maendeleo hayapaswi kusababisha uharibifu wa mazingira.

Amesema hayo jijini Nairobi, wakati akifunga mjadala kuhusu sayansi, sera na biashara, mjadala uliofanyika kwa siku mbili.

Bwana Lajčák amesema hayo akizingatia kuwa harakati za sasa za maendeleo duniani zimekumbwa na vikwazo kama vile majanga ya asili na yale yanayosabishwa na binadamu ambavyo vyote vinatishia siyo tu uwepo wa binadamu bali pia sayari dunia.