Ripoti mbili za UN zatilia shaka hatua za nchi za kupunguza joto duniani ifikapo 2030
Ingawa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa zimechukua hatua kupunguza utoaji wa hewa chafuzi, bado hatua hizo hazitoshelezi kuhakikisha kiwango cha joto duniani hakizidi nyuzi 1.5 katika kipimo cha Selsiyasi, imesema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo.