Hedhi salama

03 JUNI 2021

Hii leo jaridani tunaanza na mfumo mpya wa malipo kwa wakulima nchini Uganda kupitia MobiPay ambako sasa wakulima hawakopwi tena. Kisha suala la hedhi na changamoto zake kwa wakimbizi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Na siku ya baiskeli duniani leo tumekwenda Mwanza nchini Tanzania kuzungumza na waendesha baiskeli. Makala tunakwenda tena Uganda ambako wananchi wanataka wabunge wapya wasaidie kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Mashinani tunaelekea Sudan Kusini kwake Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Karibu!

Sauti
14'40"

28 MEI 2021

Katika Jarida la mada kwa kina hii leo Leah Mushi anakuletea
-Leo ni siku ya kimataifa ya hedhi salama ujumbe ukiwa Hatua na Uwekezaji katika Hedhi salama, wakati huu ambapo suala la hedhi linachukuliwa na jamii kuwa ni ugonjwa au mkosi na hivyo kuwakosesha watoto wa kike haki ya kupata huduma ya kujisafi wakati wa mzunguko wa hedhi kila mwezi.

Sauti
12'21"
UN/Eskinder Debebe

HER AFRICA yajitoa kimasomaso kuelimisha kuhusu hedhi salama

Suala la hedhi salama na elimu ya kifedha yamekuwa ni mambo ambayo kwa kiasi kikubwa yana mkwamo kwa watoto wa kike hususan katika nchi zinazoendelea. Kupata taulo za kike ni changamoto kubwa na hivyo kusababisha mtoto wa kike ambaye tayari amebalehe kushindwa kwenda shuleni kwa kipindi chote cha hedhi kila mwezi. Hii ni moja ya sababu zinazokwamisha lengo namba 5 la malengo ya maendeleo endelevu, SDG kuhusu usawa wa kijinsia.

Sauti
3'57"