Hii leo jaridani tunaanza na mfumo mpya wa malipo kwa wakulima nchini Uganda kupitia MobiPay ambako sasa wakulima hawakopwi tena. Kisha suala la hedhi na changamoto zake kwa wakimbizi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Na siku ya baiskeli duniani leo tumekwenda Mwanza nchini Tanzania kuzungumza na waendesha baiskeli. Makala tunakwenda tena Uganda ambako wananchi wanataka wabunge wapya wasaidie kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Mashinani tunaelekea Sudan Kusini kwake Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Karibu!