Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

haki za mtoto

Watoto wakimbizi kutoka Somalia wakiwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Daadab nchini Kenya ambako WFP inawapatia misaada ya dharura.
WFP/Rose Ogola

Majanga yanavyozidi kushamiri isiwe kisingizio cha kusigina haki za mtoto- UN

Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa hususan zile za mtoto wametoa taarifa ya pamoja hii leo huko Geneva, Uswisi wakisema  majanga ya kiafya, kibinadamu na yale  yanayohusiana na tabianchi yakizidi kuongeza changamoto kubwa duniani kila uchao kama vile ukimbizi wa ndani, ukatili wa kingono na njaa, serikali lazima zikumbuke kuwa watoto wana haki kamilifu za kimsingi za kibinadamu na kwamba haki hizo zinapaswa kulindwa.

06 OKTOBA 2022

Hii leo katika Habari za UN Assumpta Massoi anakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Kujifunza Lugha ya Kiswahili.

Katika Habari kwa Ufupi kuna haki za mtoto kuzingatiwa hasa wakati huu ambapo majanga ya kiasili na yanayosababishwa na binadamu  yanakengeua utekelezaji wa haki za mtoto. Suala la afya ya akili barani Afrika ambayo inachochea matukio ya kujiua ,na WHO imezindua kampeni maalum. Na kisha ni uzinduzi wa ripoti kuhusu matumizi ya matukio makubwa ya michezo ili kuimarisha afya ya mwili ya binadamu.

Sauti
11'26"

18 NOVEMBA 2019

Miongoni mwa Habari anazokuletea Flora Nducha katika Jarida la Habari hii leo

-Miaka 30 ya mkataba wa Haki za mtoto duniani CRC, kuna mafanikio kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF  lakini pia changamoto zinaendelea kwa watoto masikini

-Muungano wa Afrika AU na shirika la afya duniani WHO waanzisha ubia mpya ili kushirilkiana katika kutimiza malengo ya afya 

-Wakimbizi Sudan Kusini wasema wameambiwa amani imerejea Yambio sasa wanaanza kurejea nyumbani je nini wanakikuta huko?

Sauti
11'18"
Rebeca Gyumi kutoka Tanzania, mwanaharakati wa haki za wanawake na wasichana na mshindi wa tuzo ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu 2018.
UN Tanzania/ Stella Vuzo

Ushindi huu ni kwa Watoto wote wa kike Tanzania:Gyumi

Mahakama ya rufaa  kuu nchini Tanzania leo imekazia hukumu ya mahakama kuu nchini humo kwamba vifungu vya Sheria ya ndoa ya nchi hiyo vinapingana na Katiba kwa kuweka umri tofauti wa kuoa au kuolewa kati ya mtoto wa kike na wa kiume. Na hivyo kuitaka serikali kubadili sheria hiyo ambayo ni baguzi kwa watoto wa kike ndani ya mwaka mmoja.

Sauti
2'48"