Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Haiti

Watu waliohama makazi yao wakiwa katika uwanja wa ndondi katikati mwa jiji la Port-au-Prince baada ya kukimbia nyumba zao wakati wa mashambulizi ya magenge mnamo Agosti 2023.
© UNOCHA/Giles Clarke

Hali si hali Haiti, tuwasaidie polisi wa kitaifa - Türk

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu, Volker Türk, hii leo ametoa wito kwa jumuiya za kimataifa kusaidia ujumbe wa usalama kuwasaidia Polisi wa Kitaifa wa Haiti (HNP) kupambana na vurugu zinazoendelea katika ngazi zote za jamii na kuzidisha hali mbaya ya usalama na ubinadamu pamoja na mgogoro wa haki.

28 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO nchini Tanzania kwa kushirikiana na wadau wake wamewezesha hatua ya upimaji wa udongo katika wilaya sita ambako mradi wa kulinda na kuhifadhi baiyonuai unatekelezwa. Kazi hiyo imefanywa na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine - SUA, na sasa utafiti huo umekamilika, Je umebaini nini? John Kabambala wa redio washirika KidsTime ya Morogoro-Tanzania amehudhuria uzinduzi wa ripoti hiyo ya vipimo vya udongo.

Sauti
11'57"
Rais William Samoei Ruto wa Jamhuri ya Kenya akihutubia mjadala mkuu wa kikao cha 78 cha Baraza Kuu.
UN Photo/Cia Pak

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lifanyiwe marekebisho - Rais Ruto

Takwa la muda mrefu la viongozi wengi hususani kutoka Barani Afrika la Baraza la Usalama la Umoja wa lililoundwa tarehe 25 Octoba mwaka 1945 kufanyiwa marekebisho makubwa limeendelea kuchukua nafasi katika hotuba za viongozi wa ngazi za juu wanaohutubia katika mkutano wa 78 wa Baraza Kuu wa Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambapo hii leo Rais wa Kenya amesema sababu zote za kulifanyia marekebisho zipo wazi. 

Rais Joe Biden wa Marekani akihutubia Mjadala Mkuu wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani 19 Septemba 2023.
UN /Cia Pak

Idhinisheni ujumbe wa kuimarisha usalama Haiti; Biden aliambia Baraza la Usalama UN

Kuunga mkono utayari wa Kenya kuongoza ujumbe wa kipolisi unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa nchini Haiti na suala la nafasi ya umoja katika kukabili changamoto zinazokabili dunia hivi sasa ni miongoni mwa mambo aliyogusia Rais wa Marekani Joe Biden wakati akihutubia siku ya kwanza ya Mjadala Mkuu wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.

© UNOCHA/M. Minasi

Sikufahamu jinsi ya kuzungumza na mwanangu kumuepusha na mimba za utotoni - Mzazi Haiti

Hebu fikiria kutarajia kupata mtoto wakati ambapo hata hufahamu neno ujauzito lina maana gani. Hicho ndicho kilichomfika mtoto mwenye umri wa miaka 14 nchini Haiti ambaye alijikuta anapewa ujauzito na kaka wa rafiki ya kiume wa rafiki yake. Hakuwa anajitambua akakubali kumsindikiza rafiki yake na zaidi ya yote akakubali urafiki na kijana huyo mwenye umri wa miaka 16. Mama yake binti huyu naye anasema hakufahamu ni kwa jinsi gani azungumze na mtoto wake ili kumuepusha na uhusiano na wavulana kwa lengo la kumuepusha kupata ujauzito.

Sauti
4'17"
Mwanamke akiwa amesimama mbele ya nyumba yake kwenye eneo la watu waliohamishwa huko Port-au-Prince, Haiti.
IOM

Sikufahamu jinsi ya kuzungumza na mwanangu kumuepusha na mimba za utotoni- Mzazi Haiti

Hebu fikiria kutarajia kupata mtoto wakati ambapo hata hufahamu neno ujauzito lina maana gani. Hicho ndicho kilichomfika mtoto mwenye umri wa miaka 14 nchini Haiti ambaye alijikuta anapewa ujauzito na kaka wa rafiki ya kiume wa rafiki yake. Hakuwa anajitambua akakubali kumsindikiza rafiki yake na zaidi ya yote akakubali urafiki na kijana huyo mwenye umri wa miaka 16.