Pazia lafungwa, ajenda mpya ya miji yapitishwa sasa ni utekelezaji:Clos
Mkutano mkubwa kabisa wa mustakhbali wa miji duniani kwa miaka 20 ijayo, umefunga pazia hii leo mjini Quito, kwa Katibu mkuu wa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa tatu wa makazi HABITAT III kutangaza kuwa “historia imeandikwa kwa pamoja”
Joan Clos, ambaye pia ni mkurugenzi wa shirika la Umoja wa mataifa la makazi UN-HABITAT amesema mkutano huo ambao rasmi unajulikana kama mkutano wa tatu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya makazi na maendeleo endelevu mijini umekuwa wa mafanikio.
(SAUTI JOAN CLOS)