Skip to main content

Chuja:

HABITAT III

Pazia lafungwa, ajenda mpya ya miji yapitishwa sasa ni utekelezaji:Clos

Mkutano mkubwa kabisa wa mustakhbali wa miji duniani kwa miaka 20 ijayo, umefunga pazia hii leo mjini Quito, kwa Katibu mkuu wa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa tatu wa makazi HABITAT III kutangaza kuwa “historia imeandikwa kwa pamoja”

Joan Clos, ambaye pia ni mkurugenzi wa shirika la Umoja wa mataifa la makazi UN-HABITAT amesema mkutano huo ambao rasmi unajulikana kama mkutano wa tatu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya makazi na maendeleo endelevu mijini umekuwa wa mafanikio.

(SAUTI JOAN CLOS)

UN Photo/Eskinder Debebe)

Mkutano wa HABITAT III kufunga pazia Quito

Mkutano wa tatu wa makazi yaani HABITAT III unakunja jamvi hii leo mjini Quito Ecuador. Mkutano huo unamalizika kwa nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa kupitisha ajenda mpya ya miji.

Ajenda hiyo inalenga kuwawezesha wakazi wote wa mijini wakiwemo wahamiaji na wakimbizi wawe wanaishi kwenye makazi rasmi ama yasiyo rasmi kuishi maisha bora, yenye hadi na yenye faid.

Mameya wana jukumu muhimu katika ajenda mpya ya miji

Mameya wa miji mikubwa ndio hasa watakaobeba bendera linapokuja suala la utekelezaji wa ajenda mpya ya miji iliyopitishwa kwenye mkutano wa tatu wa makazi yaani HABITAT 111 mjini Quito, Ecuador.

Huo ni mtazamo wa Mark Watts, mkurugenzi mtendaji wa kundi la masuala ya mabadiliko ya tabianchi liitwalo C-40 Climate Leadership Group, ambalo linawakilisha mameya 68 wa miji mikubwa duniani.