Filamu ya Hawar kuhusu mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa jamii ya wayazidi Kaskazini mwa Iraq imeweka bayana ukatili waliofanyiwa watu hao. Tupate taarifa Zaidi na Flora Nducha
Ugonjwa wa kipindupindu na kuharisha umeongezeka mara dufu nchini Yemen mbali na zahma nyingine kama njaa, ukosefu wa mahitaji muhimu na mahangaiko ya vita kila uchao.
Licha ya kukabiliwa na shida za kiafya na usalama, mshikamano baina ya wakimbizi wa Rohingya huko Bangladesh umeleta matumaini miongoni mwao. Leah Mushi na ripoti kamili.