Mjumbe Maalumu wa KM kwa Usomali, Ahmedou Ould-Abdallah amewatumia umma wa Kisomali, uliotawanyika sehemu kadha wa kadha za ulimwengu, barua yenye kueleza kwamba chimbuko la matatizo ya taifa lao linatokana na ukosefu wa uongozi imara wa kisiasa, uongozi uliojihusisha kidhati na masuala ya kijamii, na wenye kujali majukumu ya kitaifa.