Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon ambaye anafuatilia kwa karibu hali ya Ivory Coast amesema anahofia machafuko yalivyoshika kasi nchini humo.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa kidini au imani Heiner Bielefeldt amepongeza mazingira ya uwazi na kuvumiliana nchini Paraguay katika ngazi ya jamii na serikali kwa ujumla.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon leo amezindua ofisi mpya za shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP na shirika la makazi duniani UN-HABITAT mjini Nairobi Kenya.
Mionzi ya nyuklia inayoendelea kuvuja kwenye mtambo wa Fukushima Daiichi nchini Japan umewafanya maelfu ya raia wa nchi hiyo kusalia na wasiwasi wa afya zao.
Gharama kubwa za chakula zimezuia watu milioni 19.4 katika nchi za Asia -Pacific kujikwamua na umasikini mwaka jana imesema ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa leo iitwayo uniting for universal access inasisitiza uvumilivu sufuri dhidi ya maambukizi ya HIV, ubaguzi na vifo vitokanavyo na ugonjwa huo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon kwa ushirikiano na mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Ukimwi UNAIDS Michel Sidibe leo wamezindua rasmi ripoti ya Ukimwi mjini Nairobi Kenya.