Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

guterres

22 JULAI 2025

Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika SDG17 katika mazungumzo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa na idhaa hii hivi karibuni hapa New York.  Pia tunakuletea mutasari wa habari na mashinani.

Sauti
10'53"

04 APRILI 2025

Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu mabomu ya kutegwa ardhini. Makala inamulika harakati za kusongesha malengo ya maendeleo endelevu ikitupeleka nchini Kenya na mashinani tunasalia huko huko nchini Kenya, kulikoni?

Sauti
9'59"

13 MACHI 2025

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Idhaa hii imezungumza na Lucy Gidamis, Wakili ambaye kwa sasa anafanya kazi na shirika la Msichana Initiative nchini Tanzania akijikita katika kutetea na kutekeleza haki za wanawake. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ufafanuzi wa neno Wakfu.

Sauti
11'
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres
Picha ya UN /Rick Bajornas

Madaraka na usawa vimfikie mwanamke- Guterres

Mkutano wa 62 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW umeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.

Maudhui ya mkutano huo wa wiki mbili ni changamoto na fursa katika kufikia usawa wa jinsia na kuwezesha wanawake na wasichana waishio vijijini. 

Taliban watumia gari la wagonjwa kushambulia Kabul

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali shambulio lililofanyika leo kwenye mji mkuu wa Afghanistan, Kabul ambako washambuliaji walitumia gari linalofanana na gari la wagonjwa kutekeleza shambulio hilo.

Vyombo vya habari vinaeleza kuwa watu wapatao 95 wameuawa na wengine wengi wamejeruhiwa katika shambulio hilo ambalo kikundi cha Taliban kimekiri kuhusika nalo.

Elimu ndio muarobaini dhidi ya chuki za kibaguzi

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kumbukizi ya wahanga wa mauaji ya halaiki dhidi ya wayahudi, Umoja wa Mataifa umesema silaha pekee dhidi ya vitendo kama hivyo ni elimu na uelewa kuhusu maadili ya kibinadamu.

Katibu Muu wa Umoj awa Mataifa António  Guterres amesema hayo katika ujumbe wake akieleza kuwa mambo hayo ni muhimu hivi sasa kwa kuwa hata baada ya vita kuu ya pili ya dunia, bado kuna mwendelezo wa chuki siyo tu dhidi ya wayahudi bali pia chuki kwa misingi mingine kama rangi na dini.