Serikali, asasi za kiraia pamoja na mamlaka za kikanda zimehimizwa kujitayarisha vyema kwa mkutano mkuu kuhusu uhamiaji zikiwa tayari kuweka azma kuwa zitatumia faida za uhamiaji uliosimamiwa vizuri kwa minajili ya kupunguza athari mbaya za sera mbovu na kutokuwepo ushirikiano katika suala zima la uhamiaji.