Chuja:

Glasgow

Wanaharakati kutoka makundi ya watu wa asili wameandamana katika mitaa ya jiji la Glasgow wakati wa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa tabianchi, COP26
UN News/Grace Barret

COP26: Watu wa asili wana nafasi kubwa ya pekee katika kuzuia mabadiliko ya tabianchi 

Mamilioni ya watu wameingia kwenye mitaa ya miji kote ulimwenguni ikiwa ni pamoja na viunga vya mji wa Glasgow nchini Uskochi unakofanyika Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya tabianchi COP26 wakidai hatua kubwa zaidi ya tabianchi huku nchi zinazoshiriki katika mazungumzo ya COP26 zikiwa zimeahidi kuwekeza katika masuluhisho yasiyoharibu tabianchi kupitia kilimo.  

Mabadiliko ya tabianchi ni moja ya changamoto zinazoikabili dunia. Ukanda wa Saheli kusini mwa jangwa la Sahara.
© UNDP Mauritania/Freya Morales

Kama sisi tumeweza, wengine washindwe kwa nini? – Wakimbizi Mauritania 

Hivi karibuni, siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mabadiliko ya tabianchi, #COP26 ambao hivi sasa unaendelea Glascow, Uskochi, Mshauri Maalumu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudunia wakimbizi, UNHCR kuhusu Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Andrew Harper ametembelea Mauritania kujionea jinsi wakimbizi wanavyopambana na janga la tabianchi.

Sauti
2'5"
Mabadiliko ya tabianchi yameongeza hatari ya hali ya hewa kavu, ya joto ambao inachangia kuchochea moto wa nyika
Unsplash/Mikhail Serdyukov

COP26 ikifungua pazia WMO yasema miaka 7 iliyopita imevunja rekodi ya joto duniani

Miaka saba iliyopita inaelekea kuwa ya joto zaidi kuwahi kurekodiwa sanjari na kupanda kwa kina cha bahari ni katika viwango vya kuvunja rekodi, kulingana na ripoti ya muda ya shirika la hali ya hewa duniani (WMO) ya hali ya hewa duniani kwa mwaka 2021, iliyotolewa Jleo umapili, wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26, ukifunguliwa Glasgow, Uingereza.

Moto wa nyika katika hifadhi ya taifa ya Oregon, nchini Marekani
Unsplash/Marcus Kauffman

Joto lazidi kuongezeka duniani, binadamu anyooshewa kidole

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema zinahitajika nguvu za pamoja kutoka kwa viongozi wote wa serikali duniani na kwa haraka sana ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi yanayoikabili dunia baada ya ripoti mpya ya wanasayansi kuhusu mabadiliko ya tabianchi IPCC iliyotolewa leo kubainisha kuwa shughuli za binadamu zinapeleka dunia katika madhara ya tabianchi yasiyorekebishika. 

Mkutano wa 26 wa kimataifa wa mbadiliko ya tabianchi COP26 uliokuwa ufanyike baadaye mwaka huu umehairishwa.
Unsplash/Adam Marikar

Mkutano wa mabadiliko ya tabianchi umeishaje, na nini kinafuata?

Wakuu wa nchi na serikali zaidi ya 70 , wakiwemo pia viongozi wa kikanda, mameya wa miji mbalimbali na wakuu wa mashirika mbalimbali duniani wamewasilisha hatua wanazotarajia kuchukua ili kupunguza kiwango cha hewa chafuzi ya viwandani na kuzuia dunia kuendelea kuchemka na ongezeko la joto katika mkutano wa matamanio ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi uliomalizika Jumamosi jioni.