Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ghouta

© UNICEF/UN0185404/Sanadiki

Nini uhalali wa Baraza la Usalama kwa wasyria?

Iwapo Baraza la Usalama halitatumia mamlaka yake ya kuleta amani Syria nani ataweza kufanya hivyo?

Ni moja ya kauli lukuki zilizotamalaki wakati wa kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kilichokutana leo kutathmini utekelezaji wa azimio lake namba 2401 la kutaka sitisho la mapigano nchini Syria.

Zaidi ya mwezi mmoja tangu kupitishwa kwa azimio hilo bado hali ya usalama na kibinadamu si shwari.

Umoja wa Mataifa na wadau wake wanakumbwa na mkwamo siyo tu kwenye kuwasilisha misaada ya kibinadamu, bali pia kuwahamisha wagonjwa mahututi.

Sauti
3'15"
© UNICEF/UN0185403/Sanadiki

Yai moja Ghouta ni dola 4

Choo kimoja kutumiwa na watu 200, gharama ya yai moja ni dola 4, mfuko mmoja wa mkate dola 4, ni simulizi kutoka kwa wakimbizi walioweza kukimbia kutoka eneo la Ghouta Mashariki nchini Syria.

Ni katika eneo hilo ambako makombora yanaendelea kuporomoshwa mfululizo licha ya azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la kutaka sitisho la mapigano ili huduma ziwafikie walengwa.

Sauti
2'29"
UN /Loey Felipe

Jamani jamani sikieni vilio kutoka Ghouta Mashariki- Lowcock

Mapigano huko Ghouta Mashariki nchini Syria yakiendelea kugharimu maisha ya watu, hii leo wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamepatiwa nukuu za mashuhuda ya athari za makombora yanayoendelea kuporomoshwa kwenye eneo hilo kwa mfululizo tangu tarehe 4 mwezi huu.

Mkuu wa ofisi ya Umoja wa  Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu, Mark Lowcock amesoma nukuu hizo zilizowasilishwa kwao na wafanyakazi wa kutoa misaada nchini Syria.

Katika nukuu hii Bwana Lowcock anasema kuna familia nzima inalengwa. Mama na watoto wake watatu. Wanawake wajawazito wanne.

Sauti
2'5"