COVID-19 yazidisha makadirio ya mahitaji ya kibinadamu 2021
Watu milioni 235 duniani kote watahitaji misaada ya kibinadamu na ulinzi mwakani 2021, ikiwa ni idadi kubwa zaidi kuwahi kufikiwa, amesema mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na uratibu wa misaada ya kibinadamu (OCHA) Mark Lowcock hii leo, akitaja fedha zinazohitajika kukidhi operesheni hizo kuwa ni dola bilioni 35.