Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

GHO

Mwanamke aliyefurushwa akiwa ndani ya hema kwenye kambi ya muda, Gao inayohifadhi familia 300 waliokimbia makwao Tessit, Mali kufuatia mzozo.
© UNOCHA/Michele Cattani

COVID-19 yazidisha makadirio ya mahitaji ya kibinadamu 2021 

Watu milioni 235 duniani kote watahitaji misaada ya kibinadamu na ulinzi mwakani 2021, ikiwa ni idadi kubwa zaidi kuwahi kufikiwa, amesema mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na uratibu wa misaada ya kibinadamu (OCHA) Mark Lowcock hii leo, akitaja fedha zinazohitajika kukidhi operesheni hizo kuwa ni dola bilioni 35.