Chuja:

ghasia

Wakimbizi wakisubiri kushukishwa katika eneo moja katika jimbo la Upper Nile, Sudan Kusini.
Picha: UNHCR/Jake Dinneen

Ghasia zaongezeka jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ameeleza kushangazwa na mashambulizi dhidi ya raia yanayofanywa na watu wenye silaha huku kukiwa na ongezeko la ghasia katika Jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini na kuzitaka mamlaka pamoja na viongozi wa jamii kuchukua hatua za haraka kukomesha umwagaji damu.

© UNICEF/Tanya Bindra

Matangazo ya shule kwa njia ya redio kusaidia watoto waliokimbia shule kutokana na ghasia Cameroon- UNICEF

Miaka mitatu ya ghasia na vurugu maeneo ya kaskazini magharibi na kusini magharibi mwa Cameroon zimefanya zaidi ya watoto 855,000 washindwe kwenda  shuleni, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF . Brenda Mbaitsa na ripoti kamili.

Taarifa ya UNICEF iliyotolewa leo New York, Marekani, Dakar, Senegal na Geneva Uswisi imemnukuu Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Henrietta Fore akisema kuwa bila ya hatua za dharura na kujitolea kutoka pande zote katika mzozo huo katika kulinda elimu kwa njia zote, hatma ya watoto hao iko hatarini.

Sauti
1'49"
Mwendesha mashtaka mkuu wa Mahakama ya  ICC
UN Photo/Rick Bajornas)

DRC Jiepusheni na uhalifu wakati wa uchaguzi la sivyo mtawajibishwa- ICC

Kuelekea uchaguzi mkuu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC tarehe 23 mwezi huu, mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC imeonya kuwa yeyote yule nchini humo ambaye atachochea, ama atashiriki katika fujo kwa kuamuru, kutaka ama kuhimiza au kuchangia kwa njia yoyote ile au kutenda makosa yaliyo chini ya mamlaka ya ICC atashtakiwa na kufikishwa mbele ya mahakama.