Ghasia zaongezeka jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ameeleza kushangazwa na mashambulizi dhidi ya raia yanayofanywa na watu wenye silaha huku kukiwa na ongezeko la ghasia katika Jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini na kuzitaka mamlaka pamoja na viongozi wa jamii kuchukua hatua za haraka kukomesha umwagaji damu.