Filamu ya Royal Tour Tanzania ni mkombozi wa sekta ya utalii
Hatimaye filamu ya Tanzania The Royal tour iliyotengenezwa kuonesha vivutio vya utalii katika taifa hilo la Afrika Mashariki imezinduliwa nchini Marekani huku Msemaji Mkuu serikali ya Tanzania akisema filamu hiyo itakuwa mkombozi wakati huu ambapo mataifa mbalimbali ikiwemo Tanzania zinahaha kujikwamua kiuchumi baada ya janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19.