Jukwaa la kudumu la watu wa asili ya Afrika limeng’oa nanga UN
Jukwaa la pili la kudumu kuhusu watu wenye asili ya Afrika limeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani na litaendelea hadi tarehe 2 Juni.
Jukwaa la pili la kudumu kuhusu watu wenye asili ya Afrika limeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani na litaendelea hadi tarehe 2 Juni.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mawazo mapya na njia mpya za kuondokana na zama za ukoloni ni muhimu zaidi hivi sasa ili hatimaye kuweza kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs katika maeneo 17 ambayo bado yanatawaliwa.
Kwa miaka takriban 20, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wamefanya kazi chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC -MONUSCO ili kuokoa na kubadilisha maisha katika hali tete ya kisiasa na kiusalama humo. Miongoni mwa vikosi vinavyosaidia amani nchini humo ni KEN QRF 2.
Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), James Elder amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi kwamba "watoto wengi zaidi nchini Sudan wanahitaji usaidizi wa kuokoa maisha kuliko hapo awali", huku watoto milioni 13.6 wakihitaji msaada wa haraka.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) leo Jumanne limeeleza kuwa kwa mara ya kwanza tangu mapigano yazuke nchini Sudan tarehe 15 Aprili, wahudumu wa kibinadamu sasa wameweza kufikisha msaada wa chakula kwa familia zilizokata tamaa zilizokwama katika kitovu cha mzozo huo, Khartoum.
Jaridani hii leo ni mada kwa kina leo tunaelekea nchini DRC kuangazia kikosi cha pili cha walinda amani kutoka Kenya cha kuchukua hatua za haraka KEN QRF 2 kinachohudumu mjini Beni, Jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, DRC-MONUSCO. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za matumaini kwa familia zilizokata tamaa zilizokwama katika kitovu cha mzozo nchini Sudan, msaada wa kibinadamu kwa watoto nchini humo, na wakimbizi wanaohama kwa nchi jirani.
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP, linaongeza hatua zake za dharura kusaidia mamia kwa maelfu ya Wakenya walioathiriwa na athari za takriban miaka mitatu ya ukame.
Kikosi cha 10 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANZBATT-10 kinachohudumu kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi (FIB) kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kimeadhimisha siku ya ulinzi wa amani duniani hii leo tarehe 29 Mei kwa kutembelea kituo cha watoto yatima cha DORIKA kilichopo OICHA Jimbo la Kivu kaskazini nchini DRC. Wakiwa kituoni hapo wamewapatia misaada ya kiutu watoto hao ikiwa pia ni lengo la kulinda uhusiano na ushirikiano kwenye eneo lao hilo la uwajibikaji.
Serikali ya Uganda chini ya Rais wake Yowei Museveni imepongezwa kwa juhudi za kuhakikisha wananchi wake wenye Virusi vya UKIMWI wanagundulika na kupatiwa huduma na katika kuendeleza hali hiyo imeombwa kujitafakari na kuhakikisha wananchi wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja hawaathiriki wala kunyanyapaliwa.
Ripoti - 'Maeneo yenye Njaa - FAO-WFP onyo la mapema juu ya uhaba mkubwa wa chakula' - iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula (WFP) inataka hatua za haraka za kibinadamu kuokoa maisha na njia za kujikimu na kuzuia njaa na vifo katika maeneo yenye njaa kali ambayo iko katika hatari kubwa ya kuongezeka kuanzia Juni hadi Novemba 2023.