Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Geneva

15 MACHI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea tunaangazia vurugu nchini Syria ambapo ni miaka 12 kamili tangu machafuko yalipozuka; na ripoti ya ILO inayosihi nchi zote duniani ziboreshe mazingira ya kazi ya watendaji hao. Makala tutaelekea nchini Bahrain na mashinani nchini Geneva, kulikoni?.

Sauti
13'15"
Mkono wa mtoto anayesumbuliwa na utapiamlo ameuweka kwenye mkono ya bibi yake. Mtoto anaishi Kobamirafo, umbali wa dakika 50 kutoka Kituo cha Afya cha Msingi cha Ambohimalaza, katika Mkoa wa Androy Kusini mwa Madagascar.
© UNICEF/UN0496476/Andriananten

Baa la njaa labisha hodi Madagascar huku hatari kwa watoto ikiongezeka:WFP

"Madagascar hivi sasa iko katika hatihati ya baa la njaa kwa mujibu wa tathmini ya vipimo vya hali cha chakula imefikia daraja la tano (IPC 5) katika baadhi ya maeneo au hali kama njaa, na hii kimsingi ndiyo hali pekee labda  na ya kwanza ya njaa iliyochochewa na mabadiliko ya tabianchi duniani," amesema Arduino Mangoni, naibu mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP nchini Madagascar, akitumia tathmini za ukosefu wa chakula za IPC, ambazo ndio hutumika kupima kiwango cha usaidizi wa dharura unaohitajika.

Vita dhidi ya malaria imeenda kombo tuirejeshe msitarini:WHO

Hayo yamesemwa na shirika la afya ulimwenguni WHO hii leo ikiadhimishwa siku ya malaria duniani, na kuongeza kuwa mwaka 2016 umekuwa na visa milioni 216 huku vifo 445,000 vikiripotiwa kutokana na ugonjwa huo hatari. 

Akizungumza mjini Geneva Uswis Pedro Alonso, mkurugenzi wa mpango wa kimataifa wa malaria amesema kauli mbiu ya siku ya malaria mwaka huu ni kuwa “Tayari kuitokomeza malaria” kwani kwa sasa dunia imefikia ukomo wa nini itakachoweza kufanikiwa kwa rasilimali chache iliyonazo hivyo amesisitiza kuwa mafanikio ya vita dhidi ya malaria yanahitaji

Sauti
2'11"

Yemen imesaidia sana wakati umefika kuilipa fadhila: UN

Jumuiya ya kimataifa imechagizwa kulipa fadhila kwa Yemen ambayo imeelezwa kuwa katika zahima kubwa na janga baya zaidi la kibinadamu duniani, nchi ambayo ambayo awali iliwakarimu wageni, waomba hifadhi na hata wakimbizi, sasa imejikuta njia panda mamilioni ya watu wake wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu. 

Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres mjini Geneva Uswis hii leo kwenye mkutano wa kimataifa wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya usaidizi wa kibinadamu Yemen.

Sauti
2'16"