Skip to main content

GDF

Nchini Libya wahamiaji hulalawakiwa wamebanana katika seliambazo zimejaa pomoni katika kituo chakuwazuilia cha Tariq al Sikka mjini Tripoli.
Photo: UNHCR/Iason Foounten

Kituo kipya cha UNHCR chaleta nuru kwa wakimbizi Libya

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR kwa ushirikiano na serikali ya Libya na washirika wa misaada, juma hili wamefungua kituo kipya cha wakimbizi mjini Tripoli, ili kuwapa wakimbizi hao mbadala salama badala ya kuwekwa kizuizini, wakati suluhu ya muda mrefu kama makazi ya kudumu na kuwasafirisha ikisawa.