Maroketi matatu yameanguka karibu na kituo cha wakimbizi Libya tunahofia usalama wao:UNHCR
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema linahofia usalama wa mamia ya wakimbizi na waomba hifadhi waliokusanyika katika kituo cha makutano na kuondoka (GDF) kilichopo mjini Tripoli nchini Libya.