Chuja:

Gavi

Msichana mdogo akipokea chanjo yake ya surua na polio kama sehemu ya kampeni ya chanjo ya nchi nzima nchini Afghanistan.
© WHO Afghanistan

Watoto nchi nzima ya Afghanistan wapatiwa chanjo za Surua na Polio

Zaidi ya watoto milioni 5 nchini Afghanistan wenye umri wa kuanzia miezi 9 hadi miaka 5 wamepatiwa chanjo dhidi ya surua ilhali watoto zaidi ya milioni 6 wenye umri wa kuanzia kuzaliwa hadi miaka 5 wamepatiwa chanjo dhidi ya polio katika kampeni ya kitaifa iliyoanza mwezi uliopita wa Novemba hadi tarehe 12 mwezi huu wa Desemba.

Robert Mwale, (wa 2 kushoto) amepona kipindupindu. Sasa ni tabasamu akiwa nyumbani kwake huko kijiji cha Mfufu nchini Malawi.
UNICEF Malawi

WHO na wadau wasongesha chanjo dhidi ya kipindupindu Malawi

Kampeni ya kutoa chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindipindu nchini Malawi ikiwa imeingina siku ya nne hii leo  na ikitarajiwa kumalizika kesho, shirika la Umoja wa Matiafa la afya ulimwenguni, WHO barani Afrika imesema kampeni inaendelea vizuri na imekuja wakati mzuri ambapo ni msimu wa mvua na maji yanaweza kubeba vijidudu kwa urahisi kwa hiyo kinga itasaidia kuepusha maambukizi. 

UNICEF/Daniel Msirikale

Wapanda mlima kilimanjaro kuchangisha fedha za kupamba na COVID-19

Wapanda mlima 34 leo wameanza safari ya kupanda mlima mrefu zaidi barani Afrika , mlima Kilimanjaro nchini Tanzania kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kuchagiza upatikanaji wa chanjo ya COVID-19 kwa wote. Kundi hilo linalojumuisha watu kutoka katika nyanja za biashara, serikali, wanamichezo mashuhuri na wawakilishi wa vijana linatarajiwa kuwasili kwenye kilele cha mlima huo tarehe 24 Oktoba siku ya Umoja wa Mataifa. 
(TAARIFA YA FLORA NDUCHA) 

Sauti
3'8"

04 JUNE 2020

Jaridani la Umoja wa Maitafa leo:

- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa asema Chanjo ni muhimu lakini pekee haitoshi

- Wakimbizi wa Mali nchini Niger wanapambana na janga la virusi vya corona kwa kutengeneza na kugawa sabuni na dawa ya kutakasa madoa baada ya kupatiwa mafunzo na UNHCR

-Mnufaika wa mafunzo ya FAO kuhusu mbinu bora za ufugaji nyuki aongea

Sauti
12'12"
Sindano imeandaliwa katika kituo cha umma  cha kampeni ya chanjo huko Sudani Kusini
UNMISS/Tim McKulka

Chanjo ni muhimu lakini pekee haitoshi:Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameuambia mkutano wa kimataifa kuhusu chanjo  unaofanyika leo kupitia njia ya mtandao kwamba chanjo ni muhimu sana na imeokoa maisha ya mamilioni ya watu duniani lakini peke yake haitoshi kukabiliana na majanga makubwa ya kiafya kama linaloisumbua dunia hivi sasa la COVID-19.

Sauti
2'11"