Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Gambia

10 NOVEMBA 2023

Ungana na Leah Mushi kusikia haya jaridani hii leo:

Hofu ya uhalifu wa vita ikitanda UN yataka jinamizi linaloghubika Gaza liishe.

UNMISS yawajengea wanajeshi wa Sudan Kusini uwezo kulinda haki za watoto.

UNCDF na EU katika harakati za kuwakwamua wananchi Gambia dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Na mashinani msichana ambaye ni mkimbizi wa ndani nchini Sudan.

Sauti
13'7"
UN News/ Hisae Kawamori

Kalavati 'lasogeza' huduma za afya kwa wanajamii Gambia

Nchini Gambia, Magharibi mwa bara la Afrika, kalavati au daraja dogo lililojengwa na shirika la Umoja wa Mataifa la maendeleo ya mitaji, UNCDF kwa ufadhili wa Muungano wa Ulaya (EU)ili kuunganisha maeneo mawili, Pakaliba na Baro Kunda, limesogeza huduma ya afya karibu na wakazi wa maeneo hayo. Anold Kayanda na maelezo zaidi

Sauti
1'30"
UN News/ Hisae Kawamori

Manusurua kutoka Gambia: Sitamani tena kuzamia kwenda ulaya

Kila mwaka maelfu ya wahamiaji kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Afrika hujaribu kufika Ulaya wakivuka Bahari ya Mediterania wakieleza kwenda kusaka maisha bora lakini safari hiyo inaelezwa kuwa ni hatari sana kwani maelfu ya watu hufa maji au kutoweka. 

Ni Amadou Jobe kijana ambaye akiwa na umri wa miaka 25 alianza safari ya hatari kutoka nchini Kwake Gambia kupitia kaskazini mwa Afrika lengo likiwa Kwenda nchini Italia kusaka maisha bora kwani alikuwa akiishi katika hali ya umasikini na alitamani kuja kuisaidia familia yake iwapo angefanikiwa kufika Ulaya. 

Sauti
3'19"
Amadou Jobe, mhamiaji ambaye alirejea Gambia kutoka Ulaya, akiangalia bahari ya Pasifiki kutoka pwani ya Gambia.
UN News/ Hisae Kawamori

Sitamani tena kuzamia kwenda Ulaya: Manusura kutoka Gambia

Kila mwaka maelfu ya wahamiaji kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Afrika hujaribu kufika Ulaya wakivuka bahari ya Mediterania kwa lengo la kwenda kusaka maisha bora lakini safari hiyo inaelezwa kuwa ni hatari sana kwani maelfu ya watu hufa maji au kutoweka. Evariste Mapesa anatupeleka nchini Gambia kusikia simulizi ya kijana ambaye chupuchupu apoteze maisha. 

 

Sauti
3'19"
© UNICEF/UN0624023/

Mhamasishaji wa kijadi atumikisha kuchagiza chanjo Gambia

Utoaji wa chanjo kwa watoto umekuwa unakumbwa na changamoto katika baadhi ya maeneo duniani kutokana na jamii kuwa na imani potofu na ndio maana huko nchini Gambia shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limeamua kutumia washawishi kwenye jamii ili kuhamasisha wazazi kupeleka watoto wao kupata chanjo kama anavyosimulia Assumpta Massoi. 

Tuko nchini Gambia, taifa hili lililoko magharibi kabisa kwa Afrika, ni midundo ya ngoma kutoka kwa Lamine Keita, mwanamuziki wa kitamaduni, almaaruf, Takatiti. 

Sauti
1'37"

17 Juni 2022

Hii leo Ijumaa, Leah Mushi anakuleta jarida la habari likimulika: 
1.    Watoto kutawanywa duniani kote kutokana na machafuko, taarifa kutoka UNICEF 
2.    Mhamasishaji wa kijamii atumia ngoma na kipaza sauti kuhamasisha wazazi na walezi kupeleka watoto wao kupata chanjo. 
3.    Makala anakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako Byobe Malenga amemulika utumikishaji watoto jimboni Kivu Kusini. Mtoto katoa ushuhuda. 

Sauti
11'23"

17 MACHI 2022

Miongoni mwa yaliyomo leo katika jarida letu la Habari linaloletwa kwako na Leah Mushi

- Mswada mpya unaopendekewa Uingereza kuhusu uhamiaji hauna tija kwa wakimbizi, waomba hifadhi na wahamiaji yaonya ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa na kutoa raia kwa serikali ya nchi hiyo kuufikiria upya

-Huko Gambia mradi wa mfuko wa Umoja wa Mataifa la ufadhili kwa kilimo IFAD waleta nuru kwa wakulima wa mpunga ambao pia wanafanya biashara

Sauti
13'49"