Skip to main content

Chuja:

G5

Wakazi wa Kaskazini mwa Mali.
© MINUSMA/Gema Cortes

Kujiondoa kwa Mali kwenye G5 Sahel na Jeshi la Pamoja ni 'kizuizi' kwa eneo hilo 

Uamuzi wa nchi ya Mali mnamo Mei 15 kujiondoa katika kundi la G5-Sahel na Jeshi lake la Pamoja ni "bahati mbaya" na "wa kusikitisha", Martha Ama Akyaa Pobee ambaye ni msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Afrika, katika idara  ya masuala ya Siasa, ujenzi wa amani na kulinda amani jana Jumatano ameliambia Baraza la Usalama, huku akizitaka nchi za eneo hilo kuongeza juhudi za kulinda haki za binadamu, huku kukiwa na migogoro ya muda mrefu ya kisiasa na kiusalama. 

Bintou Keita ambaye ni msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Afrika katika  masuala ya siasa na ujenzi wa amani.
UN Photo/Loey Felipe

Hali katika ukanda wa Sahel inazidi kuwa tete na wananchi ndio waathirika wakubwa-Bintou Keita.

Bintou Keita ambaye ni msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Afrika katika  masuala ya siasa na ujenzi wa amani, hii leo mjini New York ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa hali nchini Mali na neo la Sahel kwa ujumla (Burkina Faso, Mali, Mauritania, Niger and Chad) limesalia kuwa lenye hali ya kutia wasiwasi kuanzia mabadiliko ya tabia nchi yaliyosababisha ukame, kuongezeka kwa kutokuwepo kwa usalama, makundi ya vurugu, usafirishaji haramu wa watu, silaha na madawa.

Katibu Mkuu wa UN António Guterres akiwa na Mwenyekiti wa Kamisheni ya AU Moussa Faki,  mjini Addis Ababa, Ethiopia katika picha hii ya kutoka maktaba
UN /Antonio Fiorente

Huduma inayofanywa na walinda amani wa Afrika iko katika fikra zetu-Antonio Guterres.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezishukuru nchi wanachama wa Muungano wa Afrika na Kamisheni ya Muungano wa Afrika kwa kuunga mkono operesheni za amani barani Afrika akisema kuwa huduma na kujitolea kunakofanywa na walinda amani wa Afrika kuko katika fikra zetu. Guterres amesifu kazi inayofanywa na walinda amani ikiwa ni sehemu ya hotuba yake ya leo jumapili kwa wakuu wa nchi wanaokutana katika mkutano wa Muungano wa Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia.