Wanawake wajane waanzisha kikundi cha kuwasaidia wenzao walioathirika na mapigano nchini CAR
Pamoja na kukabiliwa na ubaguzi na unyanyasaji wa kingono, wanawake nchini Jamhuri ya Afrika ya kati, CAR, wamechukua hatua ya kuwapatia matumaini wenzao wanaorejea katika makazi yao walimofurushwa kutoka na mapigano katika jamii zao.