Lengo la KEN QRF 2 ni kuzuia uhalifu kabla haujatokea DRC - Luteni Kanali David Munoru
Kwa miaka takriban 20, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wamefanya kazi chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC -MONUSCO ili kuokoa na kubadilisha maisha katika hali tete ya kisiasa na kiusalama humo. Miongoni mwa vikosi vinavyosaidia amani nchini humo ni KEN QRF 2.