Skip to main content

Chuja:

FISH4ACP

14 APRILI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia wasichana waliotekwa nyara katika shule ya bweni huko Chibok Nigeria ambapo mpaka sasa 96 bado wapo utumwani, na matokeo ya mradi wa FISH4ACP nchini Tanzania. Makala tunakupeleka nchini Rwanda na Mashinani nchini Jamhuri ya Congo, Brazaville, kulikoni?

Sauti
11'30"
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO nchini Tanzania limeendesha warsha ya siku 2 kwenye mkoa wa Kigoma ulioko magharibi mwa taifa hilo kuwapatia wadau matokeo ya utafiti wa jinsi ya kuimarisha usawa wa kijinsia kwenye sekta ya uvuvi.
Idhaa ya UN

FAO Tanzania yachukua hatua kukwamua wavuvi wanawake na wanaume kupitia FISH4ACP

Nchini Tanzania, shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO kupitia  mradi  wake  FISH4ACP  limepokea matokeo ya Utafiti kuhusu Usawa wa Kinjisia katika Masuala ya Uvuvi, moja ya hoja ambayo ikitekelezwa vema itasaidia kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs hasa la kutokomeza njaa na kuondokana na umaskini.

Sauti
2'26"
Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi Tanzania
UN News

FAO Tanzania yazindua tawi la Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi TAWFA

Katika kutekeleza lengo namba 8 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kuhusu ajira za staha na ukuaji kiuchumi sambamba na namba 5 la usawa wa kijinsia, shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo duniani FAO nchini Tanzania,  limezindua tawi la tatu la Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi TAWFA kupitia mradi wake wa kukuza mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi katika ziwa Tanganyika.

Sauti
4'19"
Mradi wa FISH4ACP wa kuongeza mnyororo wa thamani katika sekta ya uvuvi umepelekwa pia mkoani Katavi kusini-magharibi mwa Tanzania.
UN Tanzania

FAO kupitia mradi wake wa FISH4ACP walenga kuwawezesha wanawake katika biashara ya uvuvi,Tanzania

Shirika la Umoja wa Mataifa la  Chakula na Kilimo FAO kupitia mradi wake wa FISH4ACP limefanya mkutano wa pili wa Kikosi Kazi cha Taifa cha kukuza mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi katika Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma lengo likiwa ni kuimarisha na kujenga mazingira rafiki kwa wanawake ili kufanya shughuli zao katika nyanja ya uchakataji, wafanyabiashara na usafirishaji na kuongeza kipato binafsi na pato la Taifa.

17 Mei 2022

Jaridani na Leah Mushi-

HABARI KWA UFUPI 

Idadi ya watoto walioathirika na uzito mdogo wa kupindukia imekuwa ikiongezeka hata kabla ya viya ya Ukraine ambayo inatishia kuitumbukiza dunia kwenye mgogoro mkubwa wa chakula imeonya ripoti mpya kuhusu watoto iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. 

==============================================================================================

Sauti
12'6"