Akiwa nchini Ethiopia kwa ziara ya siku nne, Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, Filippo Grandi amepongeza serikali kwa uwazi wake na mbinu mpya za kuboresha maisha ya wakimbizi zaidi ya 900,000 na jamii zinazowahifadhi.