Skip to main content

Chuja:

Fiji

08 AGOSTI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kinaambapo wiki ya unyonyeshaji mtoto maziwa ya mama duniani, imehitimishwa Agosti 7, au jana Jumatatu, wiki iliyosheheni matukio ya kuonesha hatua za kuhakikisha watoto wanapozaliwa wananyonyeshwa maziwa ya mama kwa faida sio tu ya mtoto bali pia mama. Nchini Kenya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na Wizara ya Afya, walikuwa na tukio la aina hiyo na shuhuda wetu alikuwa mwandishi wetu nchini Kenya.

Sauti
11'35"
Photo: FAO/Carl de Souza

Mradi wa UN Women wa M4C waleta neema kwa wanawake Pasifiki

Katika visiwa vya Pacifiki kati ya asilimia 75 hadi 90 ya wachuuzi sokoni ni wanawake na kwa kutambua umuhimu wao na mchango wao katika jamii  shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN Women liliamua kuanzisha mradi wa masoko kwa kwa ajili ya mabadiliko au M4C kwa ajili ya kuwawezesha wanawake hao na familia zao. 

Sauti
2'27"

27 NOVEMBA 2019

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Arnold Kayanda anakuletea

-Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEf lataka mkazo uweke katika kukabiliana na ugonjwa wa surua nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, likisema ugonjwa huo unakatili maisha ya watoto wengi kuliko ebola

-Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, Ishamael Beah ametaka hatua zaidi zichukuliwe ili kulinda uhai wa watoto hususan wale wanaozaliwa njiti.

Audio Duration
11'2"
Nansen Initiative, via UNOCHA

Mabadiliko ya tabianchi hayabagui

Mabadiliko ya tabianchi hayabagui wala hayachagui, yanakumba kila mahali na kila bara. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa athari zake ni dhahiri na kuna maeneo yaliyoahatarini zaidi mfano yale ya nchi za visiwa vidogo vinavyoendelea.

Na athari hizo si katika uchumi tuu bali katika nyanja mbalimbali kuanzia haki za binadamu na hata michezo. Fiji ni miongoni mwa mataifa ya visiwa vidogo vinavyoendelea ambako kwa miongo watu wamekuwa wakifurahia fukwe za kisiwa hicho kwa kujipumzisha na hata kufanya mazoezi kwa wanamichezo.

Sauti
3'33"