Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

FIFA

Kathely Rosa, mwenye umri wa miaka 19 (kati awkiwa na mpira) akiwa na wahitimu wengine wa "One Win Leads to another", programu wa michezo nchini Brazil.
UN Women/Camille Miranda

UN WOMEN kushirikiana na FIFA katika Kombe la Dunia la wanawake

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN WOMEN linashirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA katika mashindano ya Kombe la Dunia la FIFA la wanawake yanayoanza tarehe 20 Julai mpaka 20 Agosti 2023 huko nchini Australia na New Zealand ambayo yanatarajiwa kutazamwa na zaidi ya watu bilioni mbili duniani kote, ikiwa ni hadhira kubwa zaidi katika historia ya mchezo mmoja wa wanawake. 

Bi. Salma Mukansanga, Mchechemuzi wa UNICEF kwa kipindi cha miezi 12 ili kusaidia utekelezaji wa Mkakati wa Uchechemuzi chini ya UNICEF Rwanda.
©UNICEF/Steve Nzaramba

Salima Mukansanga - Kama mimi nimefika Kombe la Dunia, hakuna ambako huwezi kufika

Michuano ya fainali za Kombe la Dunia kwa mchezo wa soka kwa wanaume inaendelea nchini Qatar huko Mashariki ya Kati. Mmoja wa watu wanaong’ara katika michuano hii ni Mchechemuzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Rwanda, Salima Mukansanga, ambaye ameweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza mweusi kuwa mwamuzi au refarii katika Kombe la Dunia. Aliingiaje katika tasnia hii ya mpira wa miguu? UNICEF Rwanda ilizungumza naye kabla hajasafiri kwenda Qatar na hapa Anold Kayanda anaeleza kwa lugha ya Kiswahili kilichozungumzwa. 

Sauti
2'39"
Mazoezi ni muhimu kwa afya.
UNICEF/Vishwanathan

Mashabiki wa mpira wa miguu duniani kote tuunde timu moja dhidi ya COVID-19-WHO na FIFA

Shirikisho la soka ulimwewnguni FIFA limeungana na Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO katika kuunga mkono kampeni ya #BeActive yaani #Jishughulishe iliyozinduliwa leo katika Siku ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa ya michezo kwa ajili ya maendeleo na amani ili kuhamasisha watu kuwa na afya wakiwa nyumbani wakati huu ambao dunia inaungana katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, COVID-19, leo na kila siku.