Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

FIB MONUSCO

Ujumbe wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) watembelea vikosi vya FIB MONUSCO nchini DRC.
Abubakar Muna/JWTZ

Ujumbe wa jeshi la wananchi la Tanzania watembelea vikosi vya FIB nchini DRC

Ujumbe kutoka Tanzania ukiongozwa na Brigedia Jenerali Geoge Mwita Itang’are akiwa ameambatana na ujumbe wake kutoka makao makuu ya Jeshi la Ulinzi la wananchi Tanzania (JWTZ) kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya ulinzi ya Tanzania Jenerali John Jacob Mkunda umefanya ziara ya kutembelea makao makuu ya majeshi ya Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo  DRC ujulikanao kama MONUSCO kwenye eneo la Goma na kukutana na kamanda wa vikosi hivyo Luteni Jenerali Otavio Rodrigues De Miranda Filho.

TANZBATT 9

TANZBATT 9 wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. 

Sauti
1'45"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa, Kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 katika doria ya barabara ya Mbau-Kamango
TANZBATT 9

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. 

Sauti
1'45"
Walinda amani kutoka Tanzania waanzisha kampeni ya "Afya na Amani" nchini CRC
Picha: MONUSCO

Baada ya Mavivi, walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafikisha misaada Hospitali ya Oicha, DRC

Kikosi cha 9, TANZBATT 9 cha wanajeshi walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo DRC-MONUSCO, wameendelea na kampeni yao ya Afya na Amani ambapo hadi tarehe 13 mwezi huu wa Januari watakuwa wakiendelea kutoa misaada kwa jamii inayoishi katika eneo lao la kazi, kaskazini mashariki mwa nchi.

Sauti
2'13"
TANZBATT_8/Kapteni Tumaini Bagambo

Kutanguliza majadiliano katika kutatua matatizo ya ukosefu wa amani utarejesha amani DRC: Meja Jenerali Simuli

Meja Jenerali Paul Kisesa Simuli ambaye ni Mkuu wa Utumishi katika Jeshi la Tanzania ametoa wito kwa Raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kutanguliza majadiliano katika kutatua matatizo yao ya ukosefu wa amani. 

Meja Jenerali Simuli ametoa wito huo alipoongoza ujumbe wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika ziara yao nchini DRC ili kujionea shughuli za mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO ambamo kwa nyakati tofauti, walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wamekuwa wakihudumu katika vikosi mbalimbali kikikwemo cha kujibu mashambulizi, FIB. 

Sauti
1'46"