Skip to main content

Chuja:

Features

UN Photo/JC McIlwaine

UNICEF na wadau wawezesha watoto milioni mbili katika migogoro kuendelea na masomo

Japokuwa kumekuwa na madhara ya vita, maafa ya asili na dharura nyinginezo, takriban watoto milioni mbili katika nchi 20 kote duniani wamekuwa na uwezo wa kuendelea na masomo kwa kipindi cha miaka minne kutokana na ushirikiano kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na idara ya Tume ya Ulaya ya misaada ya kibinadamu na ulinzi wa raia.

UN Photo/Paulo Filgueiras

Uchumi unatoa fursa ya kufikia malengo ya SDG: ESCAP

Hali imara ya kiuchumi katika kipindi cha pili ya mwaka wa 2016 inatoa fursa ya kuelewa hali ya kiuchumi, kijamii, kimazingira na vipimo vya utawala ili kufikia malengo ya maendeleo endelevu ipasavyo. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya mwisho wa mwaka huu iliyo kwenye chapisho lao la utafiti la tume ya uchumi na kijamii ya Umoja wa Mataifa  kwa ukanda wa Asia-Pasifiki (ESCAP).

Ripoti hiyo inasema sera za kodi za maendeleo, utawala bora na ufanisi wa kiuchumi vinaweza kusaidia uchumi kufanya maendeleo katika kushirikisha na kuelekea kwa maendeleo endelevu.

UN Photo/Loey Felipe

Mkakati mpya wa mazingira katika ulinzi wa amani wawasilishwa

Msaidizi wa Katibu Mkuu kuhusu operesheni za ulinzi wa amani Atul Khare amewasilisha mkakati mpya wa mazingira katika uendeshaji wa operesheni za amani za Umoja wa Mataifa katika Chuo Kikuu cha Columbia hapa mjini New York Jumanne.

Bwana Khare amelezea mtazamo wa idara yake kuwa Ofisi zao kwenye maeneo mbali mbali zinawajibika kufanya kazi katika ufanisi wa kiwango cha juu katika matumizi  ya mali asili, na kutohatarisha watu, jamii na mazingira popote iwezekanavyo.

(Sauti ya Atul)

UN Photo/Eskinder Debebe)

Makundi ya waasi acheni vurugu CAR- Ban

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban ki-moon amesema ana wasiwasi juu ya vurugu mpya zilizofanyika wiki iliyopita huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR.

Taarifa ya msemaji wa Umoja wa Mataifa imeeleza kuwa wakati wa ghasia hizo makundi mawili yaliyojihami ambayo zamani yalikuwa upande wa Seleka yalipambana katika mkoa wa Bria na ambapo watu kadhaa wameuawa na zaidi ya 11,000 walikimbia makazi yao.

Wengi wa waathirika ni raia, idadi kubwa ikieleza kuwa walilengwa kwa sababu ya makabila yao.