Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la kuhudumia wakimbizi UNHCR na la uhamiaji IOM, wametoa wito kwa Muungano wa Ulaya EU na Muungano wa afrika AU, kubadilisha mtazamo kwa wakimbizi na wahamiaji nchini Libya na kutekeleza hatua kadhaa zenye lengo la kuwasaidia wakimbizi na wahamiaji waliokwama kwnye vituo mbalimbali Libya au wanaojaribu kuchukua safari za hatari kwenye bahari ya Mediterranea.