Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Elizabeth Mrema

UNDP/Ya'axche

Tusipolinda bayoanuai tunajiangamiza wenyewe:CBD

Tatizo la kutoweka kwa bayoanuai ambayo ni muhimili mkuu wa maisha ya dunia na viumbe vilivyomo linaongezeka kila uchao na mlaumiwa mkubwa ni binadamu na shughuli zake za kila siku. Mwishoni mwa wiki Dunia ikiadhimisha siku ya kimataifa ya bayoanuai iliyobeba kaulimbiu  “sisi ni sehemu ya suluhu”  Umoja wa Mataifa umetoa rai kwa kila mtu kuwajibika kuilinda bayoanuai ambayo hakuna atakayesalimika bila hiyo .

Sauti
9'5"

24 MEI 2021

-Katika jarida la mada kwa kina hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Leah Mushi anakuletea 

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mlipuko wa volkano katika mlima Nyiragongo mjni Goma jimboni Kivu Kaskazini umesababisha vifo vya watu 15. 

-Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amehutubia mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Shirika la afya la Umoja wa Mataifa Ulimwenguni, WHO na kusema iwapo ubaguzi katika utoaji chanjo dhidi ya COVID-19 utaendelea, nchi tajiri zitachanja watu wake  huku virusi vikiendelea kusambaa  katika nchi

Sauti
11'10"
UNEP

Mrema: Mimi na wewe sote tunawajibika kulinda bayoanuai

Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kwamba bayoanuai ya dunia inaendelea kupotea na endapo hatua madhubuti hazitochukuliwa sasa basi  mustakbali wa viumbe vya dunia wakiwemo binadamu, mazingira na sayari yenyewe kwa kizazi hiki na vizazi vijavyo utakuwa njiapanda.  

Umoja wa Mataifa umeendelea kuzihimiza nchi wanachama kuzingatia suala hili ambalo ni muhimu kwa kila nyanja ya maisha ukisisitiza pia “Hatua za haraka kuchukuliwa kuhusu bayoanuai kwa ajili ya maendeleo endelevu” SDGs.  

Sauti
9'50"
UN /John Isaac

Mrema: Kulinda bayonuai ni jukumu la kila mtu kwa ajili ya kizazi hiki na vijavyo

Mkutano wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaendelea mjini New York Marekani na leo unajikita na suala la bayonuai ambayo kwa muda sasa imekuwa ikiendelea kupotea na kuzusha hofu ya mustakbali wa viumbe vya dunia wakiwemo binadamu, mazingira na sayari yenyewe kwa kizazi hiki na vizazi vijavyo.  Flora Nducha amezungumza na mmoja wa wazungumzaji wakuu wa mjadala wa leo ni Bi. Elizabeth Mrema katibu mtendaji wa mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya bayonuai. 

Sauti
3'40"

30 Septemba 2020

Kulinda bayonuai ni jukumu la kila mtu kwa ajili ya kiazazi hiki na vijavyo asema Bi. Elizabeth Mrema Katibu Mtendaji wa mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya bayonuai. Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mradi ulioendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF umewezesha watoto kufungua mradi wao wa kuoka na kupika mikate, mandazi na kalmati na hivyo kuona angalau nuru ya maisha kwenye taifa hilo lililogubikwa na mizozo hususan mashariki mwa nchi. Na UNIFIL yakita kambi Beirut kusaidia kurejesha maisha ya mji huo mkuu wa Lebanon.

Sauti
13'22"