Edem Wosornu: Watu wa Haiti wanaomba mambo matatu
Wakati wa ziara ya siku nne nchini Haiti hivi karibuni, Mkurugenzi wa Uendeshaji na Utetezi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuratibu Misaada ya Dharura (OCHA), Edem Wosornu ametembelea maeneo kadhaa ya miradi ya misaada ya kibinadamu na kukutana na jamii zilizoathirika, mamlaka za Haiti, pamoja na washirika wa kitaifa, kimataifa na wa ndani, kujadili janga la kibinadamu nchini humo pamoja na mikakati zaidi ya misaada ya dharura.