Mkutano wa ngazi za juu wa ”Afrika tuitakayo” wafanyika Makao Makuu ya UN
Hii leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani kumefanyika mkutano wa ngazi za juu maalum kuangazia masuala ya maendeleo barani Afrika.
Hii leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani kumefanyika mkutano wa ngazi za juu maalum kuangazia masuala ya maendeleo barani Afrika.
Licha ya miaka miwili ya "mapambano ya kushangaza" dhidi ya janga la COVID-19, na huku kukiwa na changamoto zinazoongezeka za ulimwengu, matumaini ya kupatikana kwa maendeleo endelevu yanaendelea.” Amesema hii leo Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la masuala ya Kiuchumi na Kijamii, ECOSOC, Collen Vixen Kelapile.
Baadhi ya tulionayo hii kutoka Umoja wa Mataifa
Nchini Afghanistan, majira ya baridi kali yamebisha hodi huku wakimbizi wa ndani waliosaka hifadhi kwenye mji mkuu Kabul wakihaha kujikinga na familia zao kwenye mahema yasiyo na vifaa vya kuleta joto.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la masuala ya Kiuchumi na Kijamii, ECOSOC Collen Vixen Kelapile ameiteua Tanzania kuwa Mwenyekiti Mwenza wa Jukwaa la Saba la Wadau Mbalimbali wa masuala ya Sayansi, Teknolojia na Uvumbuzi katika kutekeleza Agenda 2030 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa.
Baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC leo limetuimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake huku dunia na Umoja wa Mataifa wakikabiliwa na changamoto kubwa zaidi za kiuchumi na kijamii na hasa mgogoro wa kiafya wa janga la corona au COVID-19 kuwahi kushuhudiwa.
COVID-19 ikiendelea inaendelea kuvuruga maisha na ustawi kote duniani, hii leo Jumatatu Umoja wa Mataifa umefanya mjadala mpana wa kisera kusisitiza suluhisho la ushirikiano wa kimataifa ili kupunguza janga wakati pia ulimwengu ukirejea katika mkondo wa kufikia Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu, SDGs.
Katika mkutano maalum kupitia njia ya mtandao uliofanyika leo Katibu Mkuu wa moja wa Mataifa, Rais wa Baraza Kuu la Umoja huo, Baraza la Usalama na baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC wamezijulisha nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu juhudi za Umoja huo katika kupambana na virusi vipya vya Corona, COVID-19 na kuendelea na kazi muhimu ya shirika hilo duniani kote.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Tijjani Muhammad-Bande ambaye alichaguliwa kuchukua wadhifa huo mnamo mwezi Septemba mwaka jana 2019, hii leo jumatatu, awewasilisha kwa nchi wanachama, vipaumbele vyake vya mwaka 2020.
Nchi zote duniani sasa zina fursa ya kipekee ya kuzungumza na kujifunza kutoka kwa wengine amesema leo Inga Rhonda king, Rais wa Baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC katika ufunguzi wa mjadala wa kila mwaka wa ngazi ya juu kuhusu malengo ya maendeleo endelevu (HLPF) ulioanza hapa mjini New york Marekani.
Mkutano wa Nne wa uchangishaji fedha kwa ajili ya maendeleo, FfD umeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ambapo Katibu Mkuu António Guterres amesema, “tunahitaji fedha zaidi ili kutekeleza na kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.”
Vijana wanaweza kuwa chachu kubwa katika utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu au SDG’s mwaka 2030 endapo wataelimishwa kujumuishwa na kupewa fursa.