Chuja:

ECOSOC

Wanafunzi wakihudhuria tukio baada ya masomo nchini Madagascar.
© UNICEF/Rindra Ramasomanana

Malengo ya Maendeleo Endelevu yanaweza kufikiwa ‘licha ya nyakati zetu mbaya: Rais wa ECOSOC 

Licha ya miaka miwili ya "mapambano ya kushangaza" dhidi ya janga la COVID-19, na huku kukiwa na changamoto zinazoongezeka za ulimwengu, matumaini ya kupatikana kwa maendeleo endelevu yanaendelea.” Amesema hii leo Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la masuala ya Kiuchumi na Kijamii, ECOSOC, Collen Vixen Kelapile. 

Jarida 18 Januari 2022

Baadhi ya tulionayo hii kutoka Umoja wa Mataifa 

Nchini Afghanistan, majira ya baridi kali yamebisha hodi huku wakimbizi wa ndani waliosaka hifadhi kwenye mji mkuu Kabul wakihaha kujikinga na familia zao kwenye mahema yasiyo na vifaa vya kuleta joto. 

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la masuala ya Kiuchumi na Kijamii, ECOSOC Collen Vixen Kelapile ameiteua Tanzania kuwa Mwenyekiti Mwenza wa Jukwaa la Saba la Wadau Mbalimbali wa masuala ya Sayansi, Teknolojia na Uvumbuzi katika kutekeleza Agenda 2030 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa. 

Sauti
14'54"
Munir Akram, Rais wa Baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC
UN/Ingrid Kasper

ECOSOC yatimiza miaka 75: UN

Baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC leo limetuimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake huku dunia na Umoja wa Mataifa wakikabiliwa na changamoto kubwa zaidi za kiuchumi na kijamii na hasa mgogoro wa kiafya wa janga la corona au COVID-19 kuwahi kushuhudiwa.

Umoja wa Mataifa Bangladesh unatoa kipaumbele kwa huduma zinazohusiana na unyanyasaji wa kijinsia katika jamii ambazo zimeathirika zaidi na COVID-19
UNDP Bangladesh/Fahad Kaizer

‘Uharaka wa kuchukua hatua’ kwa ajili ya maendeleo endelevu, ni mkubwa zaidi kuliko wakati mwingine wowote wakati janga la corona likiendelea

COVID-19 ikiendelea inaendelea kuvuruga maisha na ustawi kote duniani, hii leo Jumatatu Umoja wa Mataifa umefanya mjadala mpana wa kisera kusisitiza suluhisho la ushirikiano wa kimataifa ili kupunguza janga wakati pia ulimwengu ukirejea katika mkondo wa kufikia Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu, SDGs.  

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Tijjani Muhammad-Bande ashiriki mkutano kwa njia ya mtandao wa wanachama wa UN kuhusu virusi vya corona.
United Nations/Reem Abaza

UN yawajulisha nchi wanachama kuhusu mapambano dhidi ya COVID-19

Katika mkutano maalum kupitia njia ya mtandao uliofanyika leo Katibu Mkuu wa moja wa Mataifa, Rais wa Baraza Kuu la Umoja huo, Baraza la Usalama na baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC wamezijulisha nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu juhudi za Umoja huo katika kupambana na virusi vipya vya Corona, COVID-19 na kuendelea na kazi muhimu ya shirika hilo duniani kote.