Wahudumu wa afya kwenye kambi kubwa kabisa ya wakimbizi duniani ya Dadaab Kenya, wanajitahidi kupambana na mlipuko wa kipindupindu ambao tayari umeshakatili maisha ya watu 10 na wengine takriban 1000 wameambukizwa tangu ulipozuka mwezi uliopita ukihusishwa na mvua kubwa za El Niño.