Wakati kikao cha 65 cha baraza kuu la Umoja wa Mataifa kikikunja jamvi, rais wa baraza hilo Joseph Deiss amepongeza mkutano huo ambao amesema ulifungua njia ya kuongeza kasi ya kufikia malengo ya maendeleo ya milenia ya Umoja wa Mataifa na kuondokana na umasikini na maradhi yanayoisumbua dunia.