Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DRC Ituri

Mkuu wa Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa, Jean-Pierre Lacroix ziarani nchini DRC
MONUSCO

Heko MONUSCO na FARDC kwa kulinda raia na kupunguza ghasia za makundi yenye silaha: Lacroix

Huko Bunia, jimboni Ituri Mashariki Mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC,  Mkuu wa Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa, Jean-Pierre Lacroix, amepongeza juhudi za pamoja za walinda amani wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO na jeshi la serikali ya Congo, FARDC, katika juhudi za kulinda raia na kupunguza ghasia za makundi yenye silaha.

Sauti
2'36"

13 JUNI 2025

Katika Jarida la Umoja wa Mataifa leo Flora Nducha anakuletea

  • Umoja wa Mataifa walaani vikali mashambulizi ya Israel dhidi ya vinu vya nyuklia Jamhuri ya Iran
  • Huko Ituri Mashariki mwa DRC walinda amani wa Mpango wa Umoja wa Mataifa MONUSCO watoa huduma za afya kwa wananchi
  • Leo ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu watu wenye Ualibino katika makala utamsikia mbunge kmwenye ualibino kutoka nchini Tanzania
  • Na mashinani utasiki ujumbe wa nini kifanyike kuhakikisha ndoto za watu wenye ulemavu zinatimia Afrika
Sauti
11'7"
© UNICEF/UNI786600/Jospin Benekire.

Licha ya ukata UNICEF yajitahidi watoto nchini DRC warejee shuleni

Wakati ghasia zinazoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinaripotiwa kusababisha zaidi ya watoto milioni 1.8 kutokuweko shuleni, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF nchini humo linajitahidi kwa udi na uvumba kuhakikisha watoto wanapata elimu kwani ni haki yao ya msingi. Je ni kwa vipi? Anold Kayanda anasimulia zaidi.

Sauti
2'9"