Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DOHA Qatar

Rosemary DiCarlo akitoa taarifa kwenye Baraza la Usalama kuhusu shambulio la Israel Doha Qatar
UN Photo/Loey Felipe

Shambulio la Israel Doha Qatar laleta mshtuko, UN yataka diplomasia iheshimiwe

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo lilipewa taarifa na afisa mkuu wa masuala ya siasa wa Umoja wa Mataifa kuhusu shambulio la anga la Israel mjini Doha Qatar na kusema ni ongezeko la kutisha la mvutano lililolaaniwa kama uvunjaji wa mamlaka ya nchi unaotishia mazungumzo yanayoendelea ya kusitisha mapigano na kuachiliwa kwa mateka huko Gaza.