Matatizo ya afya ya akili ni changamoto kubwa kwa vijana na jamii:WHO
Nusu ya magonjwa yote ya akili duniani yanaaza katika umri wa miaka 14 na mengi ya hayabainiki wala kutibiwa, suala linaloweka mustakabali wa vijana wengi njia panda, limesema shirika la afya duniani WHO.