Skip to main content

Chuja:

dini

Ahmed Shaheed , mtaaam wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa dini au imani akihutubia kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa(kutoka maktaba)
UN Photo/Manuel Elías

Chuki dhidi ya Uyahudi ni sumu ya demokrasia, elimu yahitajika: Shaheed

Chuki dhidi ya Uyahudi ambayo ni sumu ya demokrasia  na tishio kubwa kwa jamii zote ni lazima ishughulikiwe na nchi zinapaswa kuwekeza katika zaidi katika kuelimisha kuhusu tishio hilo . Kauli hiyo imetolewa leo na mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa dini au imani Ahmed Shaheed alipowasilisha ripoti yake kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, kuhusu kuongezeka kwa chuki dhidi ya wayahudi.

UN Photo/Rick Bajornas)

Wanaotumia dini na imani kuleta mgawanyiko na mizozo wasipewe nafasi- Guterres

Kwa mara ya kwanza Umoja wa Mataifa inaadhimisha siku ya kimataifa ya kumbukizi ya waathirika wa ghasia zitokanazo na dini au imani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ulimwengu unapaswa kupinga na kukataa wale ambao kwa mabavu na kwa uongo wanashawishi kujenga imani potofu, kuchochea mgawanyiko na kueneza hofu na chuki. Arnold Kayanda na maelezo zaidi.

Sauti
1'43"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiweka shada la m aua huko Christchurch New Zealand kuenzi waathirika wa shambulio la Machi mwaka huu.
UN /Mark Garten

Siku ya kimataifa ya waathirika wa matendo ya vurugu yanayotokana na dini au imani yaadhimishwa kwa mara ya kwanza.

Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya kuadhimisha waathirika wa matendo ya vurugu yanayotokana na dini au imani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ulimwengu unapaswa kupinga na kukataa wale ambao kwa mabavu na kwa uongo wanashawishi kujenga imani potofu, kuchochea mgawanyiko na kueneza hofu na chuki. 

Sauti
1'43"
Mandhari ya mji wa Baku nchini Azerbaijan
Picha: wiraza ya utalii na utamaduni ya Azerbaijan

 Inawezekana kuishi pamoja kwa amani duniani:Moratino

Kuishi pamoja kwa amani ni jambo linalowezekana , lakini kurejea kwa kile kinachoitwa chuki, kunatia hofu kubwa ya utangamano. Kauli hiyo imetolewa na Miguel Angel Moratinos  ambaye ni mwakilishi wa Umoja wa Mataifa kwa ajili Muungano wa ustaarabu UNOAC  mjini Baku Azerbaijan ambako leo linaanza jukwaa la Umoja wa Mataifa kuhusu “majadiliano ya hatua dhidi ya ubaguzi, kutokuwepo kwa usawa na migogoro.”