Skip to main content

Chuja:

DESA

Usafirishaji wa bidha kwa kutumia mkokoteni, Lima Peru.
IMF/Ernesto Benavides

Juhudi za kujikwamua na COVID-19 zakumbana na kigingi, huku wagonjwa wakiongezeka:WESP 

Juhudi za kimataifa za kujikwamua kiuchumi na janga la corona au COVID-19 ziko katika tishio kubwa, huku idadi ya wagonjwa ikiendelea kuongezeka na utoaji wa chano katika nchi masikini ukidemadema na pengo la usawa likitumbukiza nyongo matarajio ya ukuaji wa uchumi kwa silimia 5.4 mwaka huu wa 2021 kwa mujibu wa ripoti ya hali na matarahjio ya uchumi duniani (WESP). 

Sauti
2'30"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres (Kulia) akihutubia mkutano wa jukwaa la usimamizi wa intaneti,IGF,unaofanyika hii leo mjini Paris Ufaransa, Kwenye Jukwaa ni Emanuel Macron wa Ufaransa na Audrey Azoulay-UNESCO
UN Photo.

Husisheni wadau kutoka kila nyanja mnapojadili kuhusu teknolojia ya intaneti-Guterres

Akihutubia mkutano wa jukwaa la usimamizi wa intaneti,IGF,unaofanyika hii leo mjini Paris Ufaransa,  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema, katika miaka 13 tangu mkutano wa kimataifa uliofanyika Tunisia mwaka 2005, dunia ya kidijitali imebadilika kwa kasi, fursa mpya zimefunguka na hivyo masuluhisho ya kidijitali yanabadili maisha ya watu na kwamba yanaweza kusongesha mbele kazi ya kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.

Sauti
2'11"