Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

davos

WEF/Pascal Bitz

Guterres atoa onyo kuwa hatuwezi kutatua zahma zinazotukabili katika dunia iliyogawanyika bila mshikamano

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia haiwezi kutatua changamoto kubwa inazokabiliwa nazo hivi sasa kuanzia mabadiliko ya tabianchi, vita ya Ukraine, mdororo wa uchumi na athari zinazoendelea za janga la COVID-19 katikia hali ya sasa ya mgawanyiko na kutokuwa na mshikamano hivyo wakati wa kufumbia macho changamoto hizi umepita na wanaochangia wawajibishwe.

Sauti
2'45"

18 JANUARI 2023

Hii leo jaridani tunakupeleka Davos Uswisi kusikiliza hotuba ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na pia kuangazia tuzo ya mwaka 2023 iitwayo Crystal Award. Makala na mashinani tunasalía huko huko, kulikoni?

Sauti
11'42"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihutubia kongamano la kiuchumi duniani WEF, mjini Davos, Uswisi.
© World Economic Forum

Hatuwezi kutatua zahma zinazotukabili katika dunia iliyogawanyika bila mshikamano: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia haiwezi kutatua changamoto kubwa inazokabiliwa nazo hivi sasa kuanzia mabadiliko ya tabianchi, vita ya Ukraine, mdororo wa uchumi na athari zinazoendelea za janga la COVID-19 katikia hali ya sasa ya mgawanyiko na kutokuwa na mshikamano hivyo wakati wa kufumbia macho changamoto hizi umepita na wanaochangia wawajibishwe.  

Sauti
2'45"
UN News/Kerry Constabile

Changamoto za sasa duniani ni za pamoja lakini utatuzi “segemnege”-  Guterres

Jukwaa la uchumi duniani likiendelea huko Davos nchini Uswisi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameweka bayana changamoto zinazokabili dunia hivi sasa akisema jawabu muhimu ni ushirikiano wa kimataifa ambao chombo anachoongoza ndio msingi wake. Assumpta Massoi na taarifa zaidi. 

Guterres amesema uchumi wa dunia unasuasua, giza nene limezingira dunia kiuchumi, kisiasa na kijamii na kutilia shaka mafanikio ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. 

Sauti
1'27"