Hali ya kibinadamu ikiwa bado tete Ukraine; Griffiths aanza jukumu aliliopewa na Guterres
Hii leo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limejulishwa kuwa Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura ya kibinadamu, OCHA Martin Griffiths tayari ameanza kuwasiliana na pande kinzani kwenye mzozo unaotokana na uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, jukumu alilopatiwa na Umoja wa Mataifa.