Skip to main content

Chuja:

David Beasely

Moja ya vikao vya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
UN/Eskinder Debebe

Hali ya Yemen haiko katika hatihati ya kuwa zahma , tayari ni zahma kubwa:UN

Yemen inahitaji kupigwa jeki kiuchumi, usitishaji mapigano na  mshikamano wa kimataifa  mbali ya msaada wa kibinadamu endapo jumuiya ya kimataifa inataka kuepuka baa la njaa na kuwa majaji wa kuamua mtoto yupi aewe chakula na yupi akose au yupi anastahili kuishi na yupi kufa, wamesema leo viongozi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa wakihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani.

 

Watoto wakiteka maji huko Douma, mji ulioko kwenye eneo la Ghouta Mashariki, nje kidogo ya mji mkuu wa Syria, Damascus.
UNICEF/Bassam Khabieh

Mkuu wa WFP ziarani Ghouta Mashariki nchini Syria

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la mpango wa chakla duniani, David Beasley yuko ziarani nchini Syria ambapo anatembelea maeneo ya Ghouta Mashariki na viunga vya mji mkuu Damascus, maeneo ambayo awali yalikuwa yamezingirwa na vikundi vilivyojihami na hivyo kukwamisha harakati za mashirika ya binadamu kufikisha misaada.