Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Darfur

Mtoto amesimama na maji yaliyokusanywa kutoka kambi ya IDP huko Nyala, Darfur. (Maktaba)
© UNICEF/Zehbrauskas

Tunatiwa hofu kubwa na mauaji ya raia wa kabila la Masalit Sudan - OHCHR

Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR leo imesema inatiwa wasiwasi mkubwa na kusikitishwa sana na ripoti kwamba Vikosi vya Msaada wa Haraka RSF nchini Sudan na wanamgambo washirika wao wa Kiarabu waliua mamia ya raia wa kabila la Masalit katika mji wa Ardamata mapema mwezi huu, katika shambulio lingine lililochochewa na misingi ya kikabila dhidi ya raia wasio Waarabu wa Masalit huko Darfur Magharibi katika miezi michache tu.

UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Wanawake na wasichana wafungwa minyororo Sudan

Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa (OHCHR) imesikitishwa sana na ripoti kwamba huko Darfur nchini Sudan wanawake na wasichana wanatekwa nyara na kushikiliwa katika mazingira ya yasiyo ya kiutu katika maeneo yanayodhibitiwa na wanamgambo waasi (RSF). Anold Kayanda na maelezo zaidi.  

Sauti
1'52"
Watu wanaendelea kuhama makazi yao kutokana na vita nchini Sudan.
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

UNCHR: 4,000 wauawa jimboni Darfur nchini Sudan, mali za raia zaharibiwa

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, linasema takriban watu 4,000 wameuawa huku mali za raia zikiharibiwa katika mapigano yanayoendelea huko jimboni Darfur nchini Sudan, mapigano ambayo yalianzia kwenye mji mkuu Khartoum miezi sita iliyopita na kusambaa hadi nje ya mji huo, kati ya jeshi la serikali (SAF) na wanamgambo wa Rapid Support Forces, (RSF).

Wanawake kutoka nchini Sudan wakitembea mahali salama Um Baru, Kaskazini mwa Darfur (Kutoka Maktaba).
UNAMID/Hamid Abdulsalam

ICC yaanzisha uchunguzi dhidi ya kuongezeka kwa ghasia Darfur Sudan

Mwendesha mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ICC amesema leo  kwamba anachunguza madai mapya ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu katika jimbo la Darfur nchini Siudan, ikiwa ni pamoja na mauaji ya hivi karibuni ya watu 87 wa jamii ya kabila la Masalit, yaliyoripotiwa kutekelezwa na vikosi vya msaada wa haraka RSF Rapid na wanamgambo wake.

Mama na binti zake wanne wanawasili Chad kutoka Sudan.
© UNHCR/Aristophane Ngargoune

Zaidi ya watu milioni 2.5 wametawanywa Sudan tangu Aprili 15: UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema inatiwa hofu kubwa na ongezeko la mahitaji ya kibinadamu miongoni mwa watu walioathirika na machafuko yanayoendelea nchini Sudan wakati idadi ya wati waliotawanywa na mgogoro huo ikiendelea kuongezeka na huku ufikishaji wa misaada ya kibinadamu ukiendelea kukabiliwa na vikwazoi vya kiusalama, kutokuwa na fursa ya kuwafikia wenye uhitaji na ukosefu wa fedha za ufadhili.